https://www.teiti.go.tz/storage/app/media/tanzania-mining-investment-forum.mp4
Imeelezwa kuwa, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko ameacha alama kubwa katika Sekta ya Madini katika kipindi chote alichokuwa Waziri wa Madini na kupelekea mabadiliko makubwa katika sekta hiyo.
Hayo yamebainishwa leo Septemba 23, 2023 na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Wadau wa Sekta ya Madini wakati Dkt. Biteko akifungua rasmi Maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini katika viwanja vya EPZ Bombambili Mkoani Geita.
Akizungumza mara baada ya salaam hizo Dkt. Biteko amesema kuwa masuala yote yaliyozungumzwa na mafanikio hayo katika Sekta ya Madini yametokana usimamizi madhubuti wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye sekta hiyo.
Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.